Wednesday, March 6, 2013

CBM WATEMBELEA KITENGO CHA VIZIWI MWAYA

Kitengo cha viziwi mwaya kilianzishwa tarehe 13.01.2009 na mwalimu Tumaini ngajilo(mtaalam wa viziwi).Mnamo mwezi Septemba 2009 kanisa la Anglikana dayosisi ya Ruaha walionyesha dhamira ya dhati ya kukisaidia kitengo hiki kwa kusaidia ujenzi wa madarasa kupitia mradi wa CBR unaofadhiriwa na CBM-AUSTRALIA. hapo ndipo mchakato ulipoanza wa kutafuta eneo litakalofaa kujenga madarasa ya viziwi.
Hapa ni wageni mbalimbali kutoka kanisa la Anglikana,CBM-AUSTRALIA,Mkurugenzi wa elimu maalum(wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi)ofisi ya elimu mkoa na wilaya,walimu na wajumbe wa kamati ta shule ambao walikuwa wakifanya tathmini ya maendeleo ya ujenzi huo tarehe 13.02.2013.

 Hapa wageni wa CBM wakiangalia darasa linalotumiwa na viziwi ambalo limegawanywa kwa ceiling board ili kupata madarasa matatu ndani ya chumba kimoja,kutoka kushoto,Mr.J.Katindasa(mwalimu mtaalam)Kirstin Lee Bostelmann(CBM-regional office of Kenya)Mr.T.Ngajilo(Mkuu wa kitengo cha viziwi),Simon Duffy(CBM-Australia).

No comments:

Post a Comment