Mr.B.Kulwa-Mkurugenzi wa elimu maalum(katikati)akiwa na walimu wa
kitengo cha viziwi Mwaya alipo watembelea tarehe 13.02.2013,Pamoja na
ziara hiyo aliambatana na wageni wa CBM-AUSTRALIA ambao ni marafiki wa
maendeleo ya elimu kwa viziwi,Pamoja na kuangalia maendeleo ya ujenzi wa
darasa la viziwi mkurugenzi alipata nafasi ya kuongea na walimu wa
kitengo cha viziwi na wasioona na kutoa utaratibu wa ufundishaji wa
wanafunzi wasioona kwamba wanatakiwa wasome wakiwa kwenye darasa maalum
bila kuwachanganya na wakawaida kuanzia darasa la kwanza mpaka la tatu.
Pia
aliona upungufu mkubwa wa walimu wataalamu na kuagiza uongozi wa
halmashauri ufanye utaratibu wa kuwahamishia walimu waliopitia mafunzo ya
elimu maalum waliopo kwenye shule za kawaida wahamie Mwaya badala ya
kuhamisha walimu wataalam waliopo kitengoni kwenda kwenye shule za
kawaida,Aliongeza kuwa atafanya utaratibu wa kuwapanga walimu wengi
zaidi Mwaya hivyo isitokee uongozi wa halmashauri kuwachelewesha kwa
makusudi kuwaleta Mwaya,Mwisho alisema Elimu maalum ni swala Mtambuka
hivyo hatawavumilia wasimamizi wa elimu wanaopuuza elimu maalum
kwasababu za maslahi binafsi badala ya kuwasaidia wanafunzi wenye
ulemavu.
No comments:
Post a Comment